KABESEjr Internet Cafe
max
kamwini
printer
Wednesday, May 1, 2013
Thursday, November 8, 2012
KASEJA AIBUKA KAMA MTAZAMAJI MAZOEZINI SIMBA
| Kaseja akiomba dua katika moja ya mechi za timu hiyo |
NAHODHA wa
Simba, Juma Kaseja kwa siku ya tatu mfululizo jana ameendelea na mgomo wake wa
mazoezi ya timu yake inayojiandaa na mchezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza wa
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, utakaopigwa kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam,
huku kukiwa kuna habari ameamua kuachana na timu hiyo.
Lakini tofauti
na siku mbili za awali, Kaseja jana alifika kwenye Uwanja wa Kinesi, ila mtazamaji
kama watazamaji wengine.
Hakufanya mazoezi,
ingawa alipoulizwa alisema yeye bado bado mchezaji wa Simba na ana mkataba na
timu hiyo.
Mwanzoni mwa
wiki ilielezwa kwamba Kaseja amewaaga wachezaji wenzake na kuwaambia yeye na
klabu hiyo basi.
Hatua hiyo
ilifuatia Kaseja kutukanwa na kutishiwa maisha na mashabiki wa Simba baada ya
mechi dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro wakimtuhumu
kufungwa mabao ya kizembe.
Lakini
tayari uongozi wa Simba umelaani vikali vurugu na vitisho alivyotolewa kipa wao
huyo namba moja, na kusema wanafikiria
kuwachukulia hatua kali watu waliomfanyia hivyo Nahodha wao huyo.
MILAN KUMNYOFOA BACARY SAGNA ARSENAL
8 November 2012Last updated at 23:44 GMT
INTER MILAN KUMNYOFOA BACARY SAGNA ARSENAL
Inter Milan ipo tayari kumnasa beki wa kulia wa Arsenal, Bacary Sagna, mwenye umri wa miaka 29, mwishoni mwa msimu.
Manchester United wampiga kasi katika jitihada zao za kumsajili kiungo
Mkenya mwenye umri wa miaka 21, anayechezea Celtic, Victor Wanyama,
ambaye alifunga bao katika ushindi wa 2-1 wa timu yake dhidi ya
Barcelona juzi.
Nyota wa Burnley, Charlie Austin anayetakiwa na Arsenal
Arsenal, Chelsea na Manchester City zimeripotiwa kutoa ofa kwa
ajili ya beki wa PSV Eindhoven, Riechedly Bazoer, mwenye umri wa miaka
16.
Beki wa pembeni wa Kibrazil, Wallace, mwenye umri wa miaka 18, yupo
mbioni kusaini Chelsea, kwa mujibu wa klabu yake ya sasa, Fluminense.
Habari kamili: Press Association
Arsenal imeungana na orodha ya klabu zinazomfuatilia mshambuliaji wa Burnley mwenye umri wa miaka 23, Charlie Austin.
The Gunners pia wako wanamtaka beki wa kushoto wa PSV na Uholanzi, Jetro Willems, mwenye umri wa miaka 18.
Manchester City inataka kumsajili kinda wa Chelsea mwenye umri wa miaka 16, Conor Hunte.
Chelsea imeripotiwa kutaka kumsajili mshambuliaji wa Vitesse Arnhem,
Wilfried Bony, mwenye umri wa miaka 23, ambaye amekuwa akiitwa 'new
Didier Drogba'.
Subscribe to:
Comments (Atom)























